Rais William Ruto ameteua kamati maalum itakayoongozwa na mkuu wa utumishi wa umma kushughulikia mara moja maswala yaliyoibuliwa na afisi ya rais mstaafu uhuru kenyatta, ikiwemo kumtengea uhuru ofisi na kuhakikisha ana wafanyikazi wake. Hayo ni kwa mujibu wa msemaji wa ikulu Hussein Mohamed ambaye mapema leo alidokeza kuwa rais William Ruto alizungumza na rais mstaafu Uhuru Kenyatta kuhusu malalamiko yaliyotolewa.
![](https://i.ytimg.com/vi/QCsOcNsr8Hg/maxresdefault.jpg)