Mwanadada Jonesia Rukyaa amepewa jukumu la kuamua mechi ya Watani wa Jadi (Simba vs Yanga) Januari 4, 2020. Itakuwa ni mechi ya 4 kuamuliwa na dada huyu kutoka Kagera.
Mechi alizochezesha.
Mtani Jembe 2014
Hii ndiyo ilikuwa mechi ya kwanza kuhukumiwa na Jonesia Rukyaa ambapo Simba iliifunga Yanga 2-0.
Ligi Kuu Februari 2016
Baada ya kuaminiwa kwenye game yake ya kwanza ya kuwachezesha Watani wa Jadi, safari hii alipewa jukumu la kuzichezesha timu hizi zenye historia ya aina yake kwenye soka labTanzania. Safari hii Simba ilikufa 2-0.
Septemba 2018
Kwa mara nyingine tena dada Jonesia alirudi kuzichezesha Simba vs Yanga mchezo wa raundi ya kwanza msimu uliopita uliomazika Simba 0-0 Yanga.
Januari 2020
Januari 4 mwaka huu Simba na Yanga zikicheza mechi ya kwanza ya ligi kwa mwaka huu na kukutana zenyewe, mwamuzi atakuwa Jonesia Rukyaa.
Matokeo yatakuwaje: Simba ?? Yanga
![](https://i.ytimg.com/vi/REIcSWP5_jE/mqdefault.jpg)