GLOBAL HABARI SEPT 21: Undani wa Ajali ya MV Nyerere/ Waliokufa Waongezeka
Idadi ya watu waliopoteza maisha kufuatia kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere, jirani na Kisiwa cha Ukara katika Ziwa Victoria, inazidi kuongezeka ambapo taarifa za hivi punde, zinaonesha kwamba miili 126 imeopolewa kutoka eneo la tukio.
Global TV imefika mpaka eneo la tukio na kushuhudia zoezi la uokoaji likiendelea, huku wingu zito la huzuni likiwa limetanda miongoni mwa watu waliowapoteza ndugu, jamaa na marafiki zao katika ajali hiyo mbaya iliyotokea Alhamisi ya Septemba 20, mchana.
Viongozi mbalimbali wamefika katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe, Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Simon Sirro na wengine wengi, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela kushuhudia zoezi la uokoaji likiwa linaendelea.
Miezi michache iliyopita, Mbunge wa Ukerewe, Joseph Mkundi aliwahi kuzungumzia suala la ubovu wa kivuko hicho bungeni mjini Dodoma, huku akitaka serikali ieleze ni lini injini mpya zitafungwa kwenye kivuko hicho kilichokuwa kinahudumia zaidi ya watu 50, 000.
Ещё видео!