KATAZO la NDEGE za KENYA AIRWAYS KUTUA TANZANIA – SERIKALI ZAKUBALIANA KUKUTANA MARA MOJA
Serikali za Tanzania na Kenya zimefikia makubaliano ya kushughulikia mzozo wa huduma ya usafiri wa anga kati ya mataifa hayo mawili.
Waziri Mkuu wa Kenya, Musalia Mudavadi ambaye pia ndiye Waziri wa mashauri ya kigeni aliandika kwenye akaunti yake ya mtandao wa 'X' kuwa alikuwa amefanya na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, January Makamba na kwamba nchi zote ziko tayari kukutana mara moja kutatua suala hilo ndani ya siku tatu.
Kwa upande wake, Waziri Makamba aliandika kwenye akaunti yake ya 'X' kuwa mamlaka katika nchi zote mbili zimejitolea kutatua suala hilo kwa mujibu wa makubaliano yaliyopo.
Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Tanzania ilikuwa imetangaza kusitisha safari za ndege za abiria za Shirika la Ndege la Kenya Airways (KQ) kuanzia Januari 22, mwaka huu.
Hatua hiyo inakuja baada ya Mamlaka ya Ndege nchini Kenya kukataa ombi la Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuruhusu ndege ya mizigo ya Air Tanzania kusafirisha mizigo kutoka Nairobi kwenda mataifa mengine.
Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Hamza Johari alisema kuwa, uamuzi wa Tanzania ulitokana na vikwazo vinavyowekwa na mamlaka za Kenya kuzuia shughuli za ndege ya abiria ya Air Tanzania.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa wamekuwa wakitafuta mamlaka ya Kenya kwa ajili ya usuluhishi bila mafanikio.
Mwaka 2020, mamlaka za Tanzania zilisimamisha safari za KQ kati ya Nairobi na viwanja vya Tanzania kama Dar es Salaam, Kilimanjaro na Zanzibar kwa kile ilichodai kuwa Kenya iliiwekea vikwazo mbalimbali vya kibiashara.
============================================================
⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI?
⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 713 750910), ( +255 783453136)
⚫️ Email: globaltvonlinenews@gmail.com
⚫️ OUR PLAYLISTS:
⚫️ MICHEZO na BURUDANI: [ Ссылка ]
⚫️ HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: [ Ссылка ]
⚫️ GLOBAL RADIO TV: [ Ссылка ]
⚫️ EXCLUSIVE INTERVIEW: [ Ссылка ]
⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: [ Ссылка ]
⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
⚫️ ANDROID:[ Ссылка ]
⚫️ iOS:[ Ссылка ]
![](https://i.ytimg.com/vi/SHrCCHStIuY/maxresdefault.jpg)