ASKARI WA JWT NA WENZAKE WATATU WAHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 30
Jeshi la polisi Mkoa wa Mtwara linamshilia Shaibu Yusuph Saidi aliyekuwa askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWT) MT.95850 na wenzake watatu wamehukumiwa kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kulawiti na kumpiga picha mhanga wakati wakimlawiti,hukun wakimrekodi video na kusambaza kwenye mitandao ya kijamii.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mtwara SACP Issa J.Suleiman amesema kuwa awali watuhumiwa hao walihukumiwa kilipa faini ya shilingi Milioni moja (1,000,000) katika Mahakama ya wilaya ya Mtwara,hivyo baadae upande wa Jamhuri walikata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara.
Amesema baada ya rufaa hiyo kusikilizwa April 03,2024 Mhakama Kuu ilibatilisha adhabu hiyo na kuwa kifungo cha miaka 30 jela na tayari washtakiwa hao wameanza kutumikia adhabu yao
![](https://i.ytimg.com/vi/SvkBpyY6uI4/maxresdefault.jpg)