Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini
amemuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camillus Wambura, kuhakikisha anasimamia kikamilifu sheria za usalama barabarani hususani katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa mwaka.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha 16 cha Baraza la wafanyakazi wa
Idara ya Jeshi la Polisi kilichofanyika jijini Dodoma ,Sagini amesema ni
vyema wananchi wakaendelea kushirikiana na serikali kupaza sauti kukemea ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na majeruhi
Ещё видео!