Vita ya maneno kati ya mbunge wa Kisesa na Waziri wa Fedha Dk Mwigulu Nchemba bado ni mbichi ambapo leo Jumatatu Februari 6,2023 Mpina amemchokonoa tena Dk Mwigulu sasa akitaka akiomba bunge lipitishe Azimio la kuitaka Serikali kupeleka bungeni taarifa ya matumizi ya fedha zilizokopwa nje ya bajeti lakini akipendekeza Waziri wa Fedha awajibike.
Akochangia leo katika taarifa ya Kamati ya Bajeti, mbunge huyo amesema Kuna kusuasua katika usimamizi wa matumizi ya fedha ndiyo maana kumekuwa na malimbikizo ya deni la Taifa ambalo litapelekea riba kubwa kwa siku za usoni na hivyo kuongeza mfumuko wa bei.
Kuhusu mbolea amesema kumekuwa na udanganyifu ndani yake na akaomba pia jambo hilo kupelekwa bungeni likajadiliwe kwa mapana.
Akijibu kuhusu suala la mbolea, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe Serikali itaendelea kutoa ruzuku ya mbolea kwani katika awamu hii suala la ufuatiliaji ni mkubwa kuliko Serikali zikizotangulia.
Ещё видео!