GLOBAL HABARI MACHI 02: KWAHERI RUGE! AAGWA NA MAELFU, BARNABA AZIMIA!
Rais John Pombe Magufuli ameungana na maelfu ya watanzania kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media group, Ruge Mutahaba aliyefariki dunia Feb 26, nchini Afrika Kusini kutokana na maradhi ya ugonjwa wa figo.
Ni mapema hii leo katika viwanja vya karemjee ambapo Rais Magufuli anaungana na watanzania, viongozi wa chama na serikali pamoja na viongozi wa dini katika kuuaga mwili wa aliyekuwa mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa clouds media group, Ruge Mutahaba katika viwanja vya karemjee jijini Dar es Salaam.
Akiongea kwa niaba ya familia mtoto wa kwanza wa marehemu, MWACHI MUTAHABA amaeeleza namna ambavyo familia ilitambua na kuthamini nafasi ya marehemu kwa Taifa kutoakana na kutumia muda mwingi kujitoa katika masuala ya kijamii ikiwemo tasnia ya habari pamoja na burudani.
Kwa upande wake Mkurugenzi mwenza wa kampuni ya Clouds Media group,Joseph Kusaga ameeleza mchango mkubwa ambao marehemu ameutoa kipindi cha uhai wake katika kuijenga tasnia ya habari na burudani nchini.
Baada ya zoezi la kutoa heshima za mwisho kukamilika katika viwanja vya Karemjee, mwili huo umesafirishwa kuelekea mkoani Kagera kwa ajili ya kuagwa tena katika viwanja vya Gymkhana na kupumzishwa katika nyumba yake ya milele kijini kwao Kiziru siku ya Jumatatu Machi 04, 2019.
#GLOBALHABARI
[ Ссылка ]... Watch More Videos here: [ Ссылка ] Watch More Videos here: [ Ссылка ] Website: www.globalpublishers.co.tz FaceBook:
www.facebook.com/globalpublishers Instagram: www.instagram.com/globalpublishers Twitter: www.twitter.com/GlobalHabari Install Global App: ANDROID: [ Ссылка ] Install Global App: iOS: [ Ссылка ]
![](https://i.ytimg.com/vi/V6JTJq3zIC4/maxresdefault.jpg)