Wendy Mrema anayekabiliwa na tuhuma za kumuua Mama yake Patricia Ibreck akishirikiana na watu wawili akiwemo mganga wa kienyeji, leo February 9, 2022 wote kwa pamoja wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro na kusomewa maelezo ya awali ya shtaka la Mauaji.
Wakili wa Serikali Grace Kabo akiwasomea Shtaka hilo watuhumiwa hao watatu mbele ya Hakimu Naomi Mwerinde, amesema watuhumiwa hao wanatuhumiwa kumuua Patrcia Ibreck Mrema aliyekuwa mfanyakazi wa hospital ya KCMC mnamo January 9, 2021 Mkoani Kilimanjaro.
Mshtakiwa namba moja Katika Shtaka hilo, ni Mganga wa Kienyeji Omary Muhmoud Rang’ambo mwenye umri wa miaka 32 mwenyeji wa Kigamboni Dar es salaam, na mshtakiwa wa pili ni Wendy Ibreck Mrema mwenye umri wa miaka 41 (Mkulima) na Mshtakiwa wa tatu ni Waziri Seleman mwenye umri wa miaka 37 Mkulima wa Korogwe.
Watuhumiwa hao wanaokabiliwa na kosa la mauaji wanadaiwa kutenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya kanuni ya adhabu Sura 16 marejeo ya 2019.
Ikumbukwe watuhumiwa hao walikamatwa na Jeshi la Polisi hivi karibuni kwa nyakati tofauti baada mwili wa Patricia Ibreck kugundulika umefichwa katika shimo lililokuwa limechimbwa karibu na nyumba yake ya kuishi Mkoani humo baada ya kutokuonekana kwa zaidi ya kipindi cha miezi kumi, huku mtoto wake ambaye ni miongoni mwa watuhumiwa wanaokabiliwa na kesi hiyo ambaye anafahamika kwa jina la Wendy Ibreck kudai kuwa mama yake yupo nchini India kwa ajili ya matibabu kwa kipindi chote hicho akiwa haonekani, jambo ambalo ndugu walikuja kushtuka baada ya kipindi cha miezi kumi kupita huku mali zinazokadiriwa kuwa na zaidi ya dhamani ya milioni mia tatu zikiwa zimeuzwa huku fedha zikiwa hazijulikani zilipopelekwa, ambapo kwa mujibu wa ndugu wa familia hiyo alisema pamoja na Wendy kuuza mali zilizokuwa nyumbani hapo bado alikuwa akionekana akiishi Maisha magumu huku akivaa nguo za mama yake na wakati mwingine akishindia maparachichi….
GADI TV ndiyo
Channel pekee inayokuwezesha kupata Habari za Kisiasa,Michezo, Kijamii, na Burudani kutoka Ndani na Nje ya Tanzania. Kwa huduma ya Matangazo au Habari pamoja na maoni na ushauri usisite kuwasiliana nasi kupitia namba za simu +255 769 780 063 au e-mail: gaditvhabari@gmail.com
Don't forget to SUBSCRIBE, LIKE, COMMENT and SHARE!!! # GADI TV
Thanks.
![](https://i.ytimg.com/vi/VUG-bBQZgoc/maxresdefault.jpg)