Katibu Mkuu UVCCM Komredi Jokate Urban Mwegelo (MNEC) akisoma Maazimio ya UVCCM ya kuwapongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
"Vijana wa Chama cha Mapinduzi kwa umoja wetu na dhati ya Mioyo yetu tunampongeza sana Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Kazi nzuri anayoifanya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi 2020-2025 na Uongozi wake umezidi Kuimarisha Muungano"
"Vijana wa Chama cha Mapinduzi kwa Umoja wetu na dhati ya Mioyo yetu, tunampongeza Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kazi kubwa anayoifanya ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi 2020-2025 na Uongozi wake umeendelea kuimarisha Muungano"
![](https://i.ytimg.com/vi/WTuUM69QO3Y/maxresdefault.jpg)