ZIKIWA zimebaki saa chache kabla ya tamasha la Wiki ya Mwananchi itakayofanyika Jumapili Agosti 4, 2024, Mashabiki wa Yanga jijini Mwanza wamefanya Dua maalum ya kuiombea timu yao na kuanza safari ya kwenda kuiunga mkono kwenye kilele hicho ambapo watakaa kuusubili mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mtani wao, Simba Agosti 8.
Mashabiki hao wamefanya Dua hiyo leo Agosti 2, mwaka huu katika bwalo la Jeshi jijini Mwanza, na kuanza safari yenye msafara wa magari matano kwenda jijini Dar es Salaam ambako wataweka kambi ya takribani siku Saba kuhakikisha wanaifunga Simba Agosti 8.
Akizungumzia safari hiyo, Mratibu wa klabu ya Yanga Mkoa wa Mwanza, Kija Malingwi amesema mashabiki hao watarejea jijini Mwanza kuanzia Agosti 9, huku akiwataka wanachama na mashabiki wa timu hiyo kuiunga mkono timu yao msimu huu.
Baadhi ya wanachama wa klabu hiyo waliohudhuria Dua hiyo, wameeleza umuhimu wa tukio hilo kwa timu ya Yanga huku wakituma salamu kwa mtani wao wakisisitiza kipigo kizito hakikwepeki.
Ещё видео!