Meneja masoko manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam Bw. Ramadhani Mohamedi amesema mradi wa DMPP wa ujenzi wa soko jipya la kisasa la Temeke stereo unaofadhiliwa na benki ya dunia utakapoanza hivi karibuni utasaidia kumaliza changamoto zote zilizopo ndani ya soko hilo.
Akiongea na kurasa leo Bw. Mohamedi amesema soko la Temeke stereo kwa sasa ni chakavu na miundo mbinu yake imeharibika jambo linalosababisha mvua inaponyesha wafanyabiashara ndani ya soko hilo kufanya biashara zao katika mazingira magumu.
Ещё видео!