AZIZ KI, CHAMA WAFUNGIWA MECHI TATU: Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania, imewafungia michezo mitatu na faini ya Shilingi 500,000 (laki tano) wachezaji Stephane Aziz Ki wa Yanga na Clatous Chama wa Simba SC kwa kosa la kukwepa kusalimiana na wachezaji wa timu pinzani kabla ya mechi yao iliyopigwa Oktoba 23, 2022.
Yanga pia imetozwa faini ya Shilingi 5,000,000 (milioni tano) kwa kosa la kutotumia mlango rasmi wakati wakiingia chumba cha kuvalia.
![](https://i.ytimg.com/vi/Y8y9ov-XufQ/mqdefault.jpg)