Arusha. Serikali imesema itagharamia taratibu zote za mazishi ya baba na watoto wake watatu waliofariki katika ajali ya moto jijini Arusha, sambamba na kukarabati nyumba iliyoungua.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Felician Mtahengerwa wakati alipotembelea msibani kutoa pole kwa ndugu na majeruhi saba waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa Mount Meru kwa matibabu.
Ajali hiyo iliyotokea jumamosi Juni 22, 2024 katika mtaa wa Olmatejoo jijini Arusha, ilisababishwa na kopyuta mpakato (laptop) iliyokuwa imechomekwa kwenye soketi ya umeme kushika moto na kuunguza kochi, huku watoto watatu wakifariki dunia kabla baba aliyefariki usiku wa kuamkia leo.
Waliofariki ni watoto Mariam Zuberi (9), Salma Zuberi (7), Bisma Zuberi (3) na baba yao Zuberi Msemo.
Ещё видео!