Maafisa wa polisi wanalalamikia ukosefu wa vifaa na fedha za kutekeleza majukumu yao. Kwenye kikao cha kutoa maoni mbele ya jopokazi la kushughulikia maslahi ya maafisa wa usalama linaloongozwa na aliyekuwa jaji mkuu David Maraga, Idara tofauti za polisi zimeratibu vikwazo vinavyozizuia kutekeleza kazi zao kikamilifu kama vile bunduki za kisasa, vifaa vya kutegua mabomu, na magari, miongoni mwa changamoto zingine. Ni kikao cha kwanza cha jopokazi la maraga kufanya vikao. jopokazi hilo liliundwa kutafuta mbinu za kuboresha utendakazi wa polisi pamoja na mishahara, na mazingira ya kazi.
Ещё видео!