Mali ya thamanI ya maelfu ya pesa iliteketea na abiria kunusurika kifo baada ya basi kushika moto na kuteketea katika eneo la Buoye kwenye barabara kuu ya Kisumu kuenda Nairobi Leo asubuhi
Akidhibitisha kısa hicho, kamanda wa polisi katika kaunti ya Kisumu Alphonce Kimathi, alibaini kuwa moto huo ulizuka baada ya gurudumu moja kulipuka saa kumi na mbili asubuhi. Hata hivyo watu arobaini na saba waliokuwa kwenye basi hilo walinusurika bila majeraha, huku wazima moto wakifanikiwa kuzima moto huo kwa muda. Basi hilo linalomlikiwa na kampuni ya Guardian lilikuwa likisafiri kutoka Nairobi kuelekea Busia wakati wa mkasa na sasa lipo katika kituo cha polisi cha Kisumu huku uchunguzi ukianzishwa.
Ещё видео!