Watu watatu wamefariki dunia na wawili kujeruhiwa akiwemo dereva, baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali na kupinduka katika eneo la Mtua, mkoani wa Lindi.
Ajali hiyo imetokea leo Julai 12, 2024 majira ya 5:45 asubuhi wakitokea kushiriki sherehe za Jubilei iliyofanyika katika Shirika la Mtakatifu Benedicto Abasia ya Ndanda wilayani Masasi mkoani Mtwara.
![](https://s2.save4k.ru/pic/YrUusQ4zJWU/maxresdefault.jpg)