Spika wa Bunge, Job Ndugai amewaagiza mawaziri kujibu maswali ya wabunge na kuacha alichokiita majibu yasiyojitosheleza
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Mei 24, 2021 bungeni, alipokuwa akizungumzia kutoridhishwa na namna mawaziri hao wanavyojibu hoja za wabunge.
Ndugia amesema wakati wote kiti kimekuwa kikiwavumilia Mawaziri hao kwa kuyaachia majibu hayo yaende kama wanavyojibu.
Awali, kabla ya kuanza kwa kipindi cha maswali bungeni, Spika alionya kwa Mawaziri wenye majibu marefu na wabunge wanaouliza maswali ya nyongeza kwa kuzunguka.
![](https://s2.save4k.ru/pic/Z72bRyfb7mM/maxresdefault.jpg)