GLOBAL HABARI APR 02: HATIMAYE MARIN HASSAN AZIKWA LEO, AACHA MAJONZI MAZITO NCHINI..
Waziri wa Habari, Sanaa utamaduni na michezo Dkt. Harrison George Mwakyembe amewaongoza waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa mtangazaji nguli nchini Tanzania Marin Hassan Marin.
Akizungumza baada ya maziko Dkt Mwakyembe amemshukuru Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa moyo wake wa kujitolea na kusaidia kufanikisha maziko ya Marin Hassan Marin.
Kwa upande wake Mkurugezi wa Shirika la utangazaji Tanzania (TBC) Dkt. Ayub Rioba amesema ni vyema kwa sasa kuyaenzi mambo mema aliyoyafanya Marin wakati wa uhai wake.
Mwili wa Marin Hassan umezikwa katika makaburi ya Mwanakwerekwe yaliyopo Unguja Visiwani Zanzibar.
Marin Hassan Marin, Nguli wa habari Nchini alifariki Aprili Mosi mwaka 2020, saa 2:40 asubuhi katika Hospitali ya Jeshi Lugalo baada ya hali yake kubadilika majira ya saa 12 asubuhi akiwa nyumbani kwake Mbezi Beach Jijini Dar es salaam.
Marine Hassan Marine alizaliwa mwaka 1972, alipata nafasi ya kuajiriwa katika Shirika la Utangazaji Tanzania miaka 15 iliyopita huku akikumbukwa kwa uchapakazi wake, kujitoa katika kazi sambamba na kuwaibua wanahabari wachanga katika Tasnia ya Habari.
UNA HABARI? WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE
(+255 784 888982)
(+255 676 229628)
Email: globaltvbest@gmail.com
abbymrisho@gmail.com
HABARI MPYA DAILY:
[ Ссылка ]
HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA:
[ Ссылка ]
GLOBAL RADIO TV:
[ Ссылка ]
EXCLUSIVE INTERVIEW:
[ Ссылка ]
Subscribe Global TV, Channel itakayokupa Habari na matukio ya kipekee nchini Tanzania
Ещё видео!