LYRICS
Nakupenda wewe pekee roho yangu / Yakulilia kweli eh njoo kwangu
Usiku silali mie nakuwaza we / Mawazo nenda rudi yakuzingira we
Mapenzi yako kweli yanifaa mimi / Maisha bila wewe kweli sijui
Mahangaiko yangu yameania patupu / Kutoka leo nimeyapiga marufuku
Chorus:
Nakupenda wewe pekee / Daima mimi na wewe
You linger in my mind / Hope you're always standing by my side
Nakupenda wewe pekee / Daima mimi na wewe
I have loved you from the start / You who holds the key to my heart
Nakupenda wewe pekee roho yako / Yapendeza kweli yanivuta kwako
Upole, ufadhila na ukarimu wa moyo / Utu bila uchoyo bali upendo kibao
Waliokutangulia hawakushiki / Hata wajaribu vipi hawakuwezi
Wala sisiti kusema ubaraka kwangu / Mvumilivu bila shaka hula bivu
Chorus:
Nakupenda wewe pekee sina hofu / Maisha yetu pamwe kweli si mabovu
Pawe balaa, fununu, chuki na siasa / Tukiwa pamoja yote hayo sawa sawa
Bahati nzuri tunalo pendo hili / Mwenyezi Mungu naye atubariki
Tukae pamoja siku nenda siku rudi / Katika pendo hili mi na wewe mpenzi
Chorus:
Ещё видео!