VYAMA 15 VYAUNGANA KUIPINGA CHADEMA BAADA YA KUKATAA RIPOTI YA KIKOSI KAZI
Muungano wa vyama 15 vya siasa nchini, umepinga hatua ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kukosoa na kuwahimiza wananchi kupinga yaliyowasilishwa kwenye ripoti ya kikosi kazi kilichoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan mapema mwaka huu, kwa ajili ya kutafuta muafaka wa kitaifa wa vyama vya kisiasa.
Vyama hivyo ni pamoja na ADA TADEA, CCK, DP, TLP, UPDP, AAFP, UMD, SAU, NRA, UDP, NLD, Demokrasia Makini, ADC.
Akiwasilisha hoja za vyama hivyo Katibu Mkuu wa chama cha ADC na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Baraza la Vyama cya Siasa, Doyo Hassan Doyo, amesema Chadema imeonyesha Ubinafsi wa hali ya juu, kwa kuwa ni wazi kuwa kilisusia vikao vya wadau wa siasa jijini Dodoma, huku wakituhumu kuwa hawawezi kukaa meza moja na msajili wa vyama vya siasa kutafuta muafaka.
Amesema licha ya wadau wengine kushiriki na kuja na maazimio, Chadema waliyapinga wakiwa nje ya maashauriano, na kuwa hawajafanya tafiti au kuisoma kwa kina ripoti hiyo ambayo imewasilishwa kwa rais.
WATCH WASAFI TV📺
AZAM - 411 | DSTV - 296 | ZUKU - 028 | STAR TIMES - 444 & 333 | COCONUT TV - 20 | DODOMA CABLE - 113
LISTEN WASAFI FM 📻
88.9 DAR/ZNZ/PWANI 📻 | 104.1 DODOMA 📻 | 94.5 ARUSHA 📻 | 97.3 MBEYA 📻 | 94.9 MWANZA 📻 | SHINYANGA 106.3 📻 | KIGOMA 101.7 📻
Follow Us On:
INSTAGRAM: [ Ссылка ] || [ Ссылка ]
TWITTER: [ Ссылка ] || [ Ссылка ]
FACEBOOK: [ Ссылка ]
𝑪𝒐𝒑𝒚𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕 ©2021 𝑾𝒂𝒔𝒂𝒇𝒊 𝑴𝒆𝒅𝒊𝒂. 𝑨𝒍𝒍 𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕𝒔 𝒓𝒆𝒔𝒆𝒓𝒗𝒆𝒅.
#wasafi #wasafitv #wasafifm
Ещё видео!