Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa leo hii ametembelea katika jengo la hospitali ya rufaa ambayo ni ya kanda ya kusini, jengo hilo limeanza kujengwa mwaka 2009 na mwaka 2016 kiongozi wa mbio za mwenge George Jackson aliweka jiwe la msingi. Byakanwa amesema kuwa Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania Dr Magufuli ametoa shilingi bilioni 15 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo hilo.
![](https://i.ytimg.com/vi/bZt-WWReGac/maxresdefault.jpg)