Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Geita Ndugu Nicholaus Kasendamila amewataka viongozi na wanachama wote wa Chama hicho kuendelea na kufanya kazi mbalimbali za kukiimarisha Chama ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa Ofisi za CCM za Matawi na Kata pamoja na kuanzisha miradi mbalimbali ya Uchumi ili kuendelea kukijenga Chama pamoja na Tanzania
Mwenyekiti Kasendamila alikuwa mgeni Rasmi wakati wa kuzindua Sherehe za miaka 46 ya Kuzaliwa kwa CCM ambapo Kimkoa sherehe zimefanyika wilaya ya Bukombe tarehe 01/02/2023
![](https://i.ytimg.com/vi/b_MGTnihaKo/maxresdefault.jpg)