Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara Dr Joachim Eyembe akikabidhi vifaa vya upasuaji wa mifupa kwa Daktari bingwa wa mifupa Dr Elias Godfrey vyenye thamani ya Shilingi milioni 40 ikiwa ni sehemu ya vifaa vinavyohitajika vinavyokadiriwa kufikia gharama ya jumla ya shilingi milioni 200 ambavyo vimenuniliwa kwa fedha za makusanyo ya Hospitali.
Akikabidhi vifaa hivyo Dr Eyembe amesema kua upasuaji wa mifupa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara umeanza rasmi hivyo anawakaribisha wananchi wa Mkoa wa Mara na mikoa ya jirani kufika na kupata huduma hii.
Baadhi vilivyonunuliwa ni;
1. Mashine ya umeme ya kutobolea mifupa (electric drilling machine)
2. Set za plate kubwa na ndogo za kuwekea vyuma ndani ya mfupa
3. Vitanda vya wagonjwa wa mifupa (Orthopaedic beds)
4. Set ya za antena (external fixator)
5. Vifaa vya kukatia miguu (Amputation set)
![](https://i.ytimg.com/vi/d_RLNPvtjZk/maxresdefault.jpg)