Mabawabu na walinzi wa kibinafsi sasa wana kila sababu ya kutabasamu baada ya serikali kuratibu mshahara wao wa chini kabisa kuwa shilingi 30,000. Halmashauri ya kuangazia utendakazi wa walinzi umeratibu mishahara hiyo ikisema kuwa kampuni zote zipatazo 2000 zinazotoa huduma za mabawabu zitalazimika kufuata sheria hiyo la sivyo watatozwa faini au hata kupokonywa lesieni. Na kama anavyoarifu hassan mugambi, hatua hii sasa inamaanisha kuwa, Wakenya wanaotumia huduma za mabawabu sasa watalipa gharama Zaidi.
![](https://i.ytimg.com/vi/dvZ-eQYfbaE/maxresdefault.jpg)