GLOBAL HABARI APRIL 24: WAGONJWA 37 WAPONA CORONA TANZANIA, WENGINE 108 KURUHUSIWA..
Jumla ya watu 37 waliokuwa wamekumbwa na maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona wameruhusiwa kurejea nyumbani kufuatia afya zao kuimarika baada ya kupatiwa matibabu kwenye vituo maalumu vya uangalizi.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu wakati akipokea msaada wa kusaidia mapambano dhidi ya virusi vya corona kutoka makampuni ya AZANIA ambapo jumla ya ndoo 300 za sabauni zimetolewa na Pesa taslimu milioni hamsini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Makampuni ya Azania amesema lengo la kutoa msaada huo ni kuunga mkono jitihada za Serikali kwenye mapambano dhidi ya virusi vya corona.
Katika hatua nyingine Waziri Ummy amebainisha kuimarika kwa afya za wagonjwa 108 ambao wanafanyiwa uangalizi maalumu wa kuruhusiwa huku akitoa wito kwa jamii kutowanyanyapaa watu wanaogundulika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo
Kuhusiana na sakata la uvumi wa baadhi ya wagonjwa wa corona kutoroka kwenye hospitali ya Amana, Waziri Ummy amesema hakuna mgonjwa aliyetoroka bali kumekuwepo baadhi ya wagonjwa wanaolazimisha kutaka kupewa ruhusa kutejea nyumbani.
Msomaji ni Felista Massae
Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:
ANDROID:[ Ссылка ]
iOS:[ Ссылка ]
UNA HABARI? WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE
(+255 784 888982)
(+255 676 229628)
Email: globaltvbest@gmail.com
abbymrisho@gmail.com
HABARI MPYA DAILY:
[ Ссылка ]
HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA:
[ Ссылка ]
GLOBAL RADIO TV:
[ Ссылка ]
EXCLUSIVE INTERVIEW:
[ Ссылка ]
Subscribe Global TV, Channel itakayokupa Habari na matukio ya kipekee nchini Tanzania
[ Ссылка ]
Ещё видео!