#Askarisaba#Mauaji#MuuzaMadini
Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara limekiri kuwa askari wake Saba (7) wanatuhumiwa kutekeleza mauaji dhidi ya kijana Mussa Hamisi (25), mkazi wa kijiji cha Ruponda wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi, yanayosadikiwa kufanyika Januari Tano mwaka huu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara kamishna msaidizi wa Polisi Mark Njera, amesema kwa mara ya kwanza kijana huyo alikamatwa na Polisi Oktoba 20 mwaka 2021 katika nyumba ya kulala wageni ya Sadina iliyopo Manispaa ya Mtwara Mikindani, akitokea jijini Dar es Salaam na baada ya upekuzi akakutwa na fedha shilingi Milioni 2.3, ambapo baada ya kupekuliwa zaidi nyumbani kwake Ruponda zikapatikana jumla ya shilingi Milioni 33.7.
![](https://i.ytimg.com/vi/fCqoyHRhKq0/maxresdefault.jpg)