#Kesiyaaskaripolisi#Mahakamayamtwara
Maafisa Saba wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara wanaokabiliwa na kesi ya Mauaji wa Mfanyabiashara wa Madini Mussa Hamisi Hamisi (25), mkazi wa Ruponda wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Mtwara kwa ajili ya kesi hiyo namba 01 ya mwaka 2022 kutajwa kwa mara ya Tatu.
Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Lugano Kasebele, ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 08 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa tena.
Maafisa waliofikishwa Mahakamani ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje,(aliyekuwa OC-CID),wilaya ya Mtwara, Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango,(aliyekuwa OCS) kituo cha Polisi Mtwara, Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza (aliyekuwa Mkuu wa Intelejensia ya Jinai mkoa wa Mtwara).
Wengine ni Mkaguzi wa Polisi John Msuya (Aliyekuwa Mganga Mkuu Zahanati ya Polisi Mtwara), Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.
![](https://i.ytimg.com/vi/fK1GIOU6n-w/maxresdefault.jpg)