Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan
ameridhia mapendekezo ya nyongeza ya mshahara ikiwemo kima cha chini kwa
watumishi wa umma kwa 23.3%.
Mapendekezo hayo yaliyowasilishwa Ikulu ni mwendelezo wa kikao cha Mhe.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alichofanya hivi karibuni mkoani Dodoma na
kupokea taarifa ya wataalamu kuhusu nyongeza ya mishahara.
Nyongeza hiyo imefanyika kwa kuzingatia Pato la Taifa (GDP), mapato ya ndani
yanayotarajiwa kukusanywa katika mwaka 2022/2023 na hali ya uchumi wa ndani
na nje ya nchi.
Kutokana na hatua hiyo katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imepanga
kutumia kiasi cha Shilingi trilioni 9.7 kwa ajili ya kugharamia malipo ya mishahara
ya watumishi wote katika Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi na Wakala za Serikali
Follow us on:
FACEBOOK;
SpotiLeo: [ Ссылка ]...
HabariLeo: [ Ссылка ]
DailyNews: [ Ссылка ]
INSTAGRAM;
HabariLeo: [ Ссылка ]...
SpotiLeo: [ Ссылка ]...
TWITTER;
Twitter HabariLeo: [ Ссылка ]
Ещё видео!