Mkazi wa Mwitikira, Kitongoji cha Mgumwa wilayani Bahi, Mkoa wa Dodoma, Sophia Peter Thadei (27) ameeleza namna alivyompoteza mtoto wake Gooluck Mathias wa miaka mitano kwa kunyongwa na mumewe ambaye ni baba wa kambo wa mtoto huyo usiku wa Julai 7, 2024.
Mwananume huyo, Stephano Mabula maarufu Mungo (44) inadaiwa alifanya mauaji hayo kutokana na wivu wa mapenzi kwa kumtuhumu mkewe kuwa anatembea na baba mwenye nyumba.
Imeandaliwa na Hamis Mniha
![](https://i.ytimg.com/vi/hQzdqcvWqMM/maxresdefault.jpg)