Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby wakati akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2024 / 2025 jijini Dodoma leo, amesema ikiwa itabainika kuna asilimia mbili ya madereva bodaboda ambao wamesomea udereva wao basi atachukuwa uwamuzi wa kujiuzulu.
Shabiby amesema asilimia 95 ya dereva bodaboda nchini hawana leseni huku akibainisha sababu ni gharama wanazotakiwa kutoa Sh70,000 kwa ajili ya leseni na Sh50,000 kwa ajili ya kusomea udereva huo.
![](https://s2.save4k.ru/pic/huSjGdkStts/maxresdefault.jpg)