KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA MORNING GLORY (THE SCHOOL OF HEALING) 22/ 08/ 2024
UJUMBE WA LEO: UPONYAJI WA MOYO ULIOJERUHIKA
Yeremia 33 : 6
Mithali 4 : 23
MAMBO YANAYOSABABISHA MAJERAHA NDANI YA MOYO
1. Kuchelewa kujibiwa Maombi yako
Mithali 13 : 12
12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.
2. Kubakwa
2 Samweli 13 : 14 - 16
14 Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.
15 Kisha Amnoni akamchukia machukio makuu sana; kwa kuwa machukio aliyomchukia yakawa makuu kuliko yale mapenzi aliyokuwa amempenda kwanza. Amnoni akamwambia, Ondoka, nenda zako.
16 Naye akamwambia, Sivyo, kwa kuwa mabaya haya ya kunitoa ni makuu kuliko yale uliyonitendea. Lakini alikataa kumsikiliza.
3. Kutoa mimba
4. Mahusiano kuvunjika ( uchumba na ndoa)
5. Kukataliwa
6. Kubagua Watoto
Mwanzo 37 : 1
1 Yakobo akakaa katika nchi aliyosafiri baba yake, katika nchi ya Kanaani.
7. kunyimwa haki yako
1 Korintho 7 : 3 - 5
3 Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
4 Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.
5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
8. Kusingiziwa Uongo
Ayubu 34 : 6
6 Nijapokuwa mwenye haki, nimehesabiwa kuwa mwongo; Jeraha yangu haiponyeki, nijapokuwa sina makosa.
9. Jeraha kwa sababu ya kutenda mema
Zaburi 109 : 4 - 5
4 Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa naliwaombea.
5 Wamenichukuza mabaya badala ya mema, Na chuki badala ya upendo wangu.
Mithali 22 : 6
6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
MAGONJWA YA MWILI YANAYOTOKANA NA JERAHA LA MOYO
1 Ubovu wa mifupa( Mifupa kusagika)
Zaburi 6 : 2 - 4
2 Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.
3 Na nafsi yangu imefadhaika sana; Na Wewe, Bwana, hata lini?
4 Bwana urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
Mithali 17 : 22
22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri; Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.
Mithali 14 : 30
30 Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; Bali husuda ni ubovu wa mifupa.
2.Macho kuharibika
Zaburi 6 : 4, 6 - 7
4 Bwana urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
3.Kuishiwa nguvu za mwili
Zaburi 38 : 5 - 10
5 Jeraha zangu zinanuka, zimeoza, Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimepindika na kuinama sana, Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
7 Maana viuno vyangu vimejaa homa, Wala hamna uzima katika mwili wangu.
8 Nimedhoofika na kuchubuka sana, Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako, Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.
10 Moyo wangu unapwita-pwita, Nguvu zangu zimeniacha; Nuru ya macho yangu nayo imeniondoka.
4. Ngozi ya Uso kuharibika
Mithali 15 : 13
13 Moyo wa furaha huchangamsha uso; Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
Mithali 14 : 10, 13
10 Moyo huujua uchungu wa nafsi yake, Wala mgeni haishiriki furaha yake.
11 Nyumba ya mtu mbaya itabomolewa; Bali hema ya mwenye haki itafanikiwa.
12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
13 Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni; Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.
Mhubiri: Mwl. Davidney Kaale
Kwa maombi na ushauri :
Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
Mch. Msaidizi: Anna Kuyonga
Simu: +255 713 553 443
YouTube: Kijitonyama Lutheran church
Barua Pepe: Kijitonyamalutheran@gmail.com
Ещё видео!