Naibu Waziri Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Zainab Katimba akizungumza katika kituo cha afya Ngurukua Mkoani Kigoma amepiga marufuku kuwatoza faini wajawazito ambao wamejifungulia nje ya kituo cha afya kwa dhalura ambapo atakaebainika au kuhusika hatua atachukuliwa hatua
hatua hiyo imetokana na malalamiko ya wananchi kudai kutozwa faini ya 40,000 mpaka 50,000 pindi wanaporipoti katika vituo hivyo
“ni marufuku kuwa na taratibu za kutoza wananchi faini za namna hiyo hazikubaliki kwanza ni kinyume cha miongozo hata ya sera ya afya Nchini hamna utaratibu wa kumwambia mwanamke ambaye amepatwa na dharula au mazingira aliyokuwa nayo yamesababisha ajifungue nje ya kutuo cha afya na yule yeyote ambaye atabainika kuhusika na utaratibu wa aina hiyo atachukuliwa hatua” Naibu Waziri katimba
![](https://s2.save4k.ru/pic/j8DcDjj8GnM/maxresdefault.jpg)