Mbunge wa Kisesa (CCM) Luhaga Mpina alivyotoa marekebisho zaidi ya 10 kwenye vifungu vya muswada wa Sheria ya Ununuzi wa Umma 2023 wakati wa mkutano wa 12 wa bunge la 12 bunge likiwa limeketi kama kamati ya Bunge zima.
Mkutano huo umehitimishwa leo Ijumaa, Septemba 8, 2023 ambapo Wakati akitoa hoja ya kuahirishwa kwa shughuli za Bunge Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa miswada mitatu imesomwa bungeni ambayo ni muswaada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 2 wa mwaka 2023, muswada wa sheria ya ununuzi wa umma wa mwaka 2023, pamoja na muswaada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 2 wa mwaka 2023 uliowasilishwa kwa hati ya dharura.
![](https://s2.save4k.ru/pic/lOb28urlMeM/maxresdefault.jpg)