Chama cha soka Wilaya ya Ilala IDFA kimehitimisha kozi ya makocha ngazi ya awali Grass Roots kwa wahitimu 31 kupata vyeti tayari kuanza kazi ya kuwafundisha vijana mchezo wa mpira wa miguuu.
Akiongea na waandishi wa Habari wakati wa kufunga kozi hiyo Mtendaji mkuu wa bodi ya ligi Almasi Kasongo amewapongeza washiriki hao kwa mafunzo waliyopata ambayo yatawasaidia kufanya kazi zao kwa ufanisi huku akiwaahidi vifaa washiriki watano wanawake waliyohitimu mafunzo hayo.
Kozi hiyo ya siku tano iliyoanza Septemba 19, 2022 ilihitimishwa na wanafunzi 31 huku watano (5) kati ya hayo wakiwa ni wakike.
Ещё видео!