Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema kwa mujibu wa ufuatiliaji wa wataalam walioko mkoani Lindi juu ya ugonjwa wa homa ya Mgunda uliotolewa taarifa Julai 18 mwaka huu, inaonesha kuwa toka tarehe 18 Julai 2022 hadi sasa hakujawa na mgonjwa mpya aliyeonesha dalili za ugonjwa huo. Hivyo hadi kufikia asubuhi ya leo Julai 29, 2022, idadi ya wagonjwa waliothibitishwa kuugua ugonjwa huo nchini ni 20 na na kati yao 3 wamefariki.
Waziri Ummy amebainisha hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akitoa tathmini ya ugonjwa huo, ambapo amesema wagonjwa wote wameruhusiwa kurudi nyumbani na wanaendelea na vizuri na kuwa ugonjwa huo unatibika kwa kutumia dawa ambazo zinapatikana katika vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini. Aidha, timu ya ufuatiliaji imebaini kuwa, miongoni mwa watu waliotangamana na wagonjwa hao hakuna aliyeonyesha dalili za ugonjwa huo hadi kufikia sasa.
WAZIRI UMMY ATOA TAARIFA MPYA KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA MGUNDA...
WATCH WASAFI TV📺
AZAM - 411 | DSTV - 296 | ZUKU - 028 | STAR TIMES - 444 & 333 | COCONUT TV - 20 | DODOMA CABLE - 113
LISTEN WASAFI FM 📻
88.9 DAR/ZNZ/PWANI 📻 | 104.1 DODOMA 📻 | 94.5 ARUSHA 📻 | 97.3 MBEYA 📻 | 94.9 MWANZA 📻 | SHINYANGA 106.3 📻 | KIGOMA 101.7 📻
Follow Us On:
INSTAGRAM: [ Ссылка ] || [ Ссылка ]
TWITTER: [ Ссылка ] || [ Ссылка ]
FACEBOOK: [ Ссылка ]
𝑪𝒐𝒑𝒚𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕 ©2021 𝑾𝒂𝒔𝒂𝒇𝒊 𝑴𝒆𝒅𝒊𝒂. 𝑨𝒍𝒍 𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕𝒔 𝒓𝒆𝒔𝒆𝒓𝒗𝒆𝒅.
#wasafi #wasafitv #wasafifm
Ещё видео!