WABUNGE wa bunge la Afrika Mashariki, (EALA) wamekuwa na maoni tofauti juu ya mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2021/2022 baada ya wengine kuona bajeti hiyo imeporomoka hivyo kutilia mashaka endepo shughuli za jumuiya hiyo zitatekelezwa kama zilivyo pangwa.
Kwenye bajeti ya mwaka huu iliyosomwa na Waziri Mdogo anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki kutoka Kenya,
zimeombwa jumla ya dola za Marekani 91,784,296 ikiwa ni kiwango kidogo ukilinganisha na bajeti iliyopitishwa kwa mwaka 2020/2021 ya Dola za Marekani 97,667,707.
![](https://i.ytimg.com/vi/n0yasX0WnKo/mqdefault.jpg)