Uongo na Ukweli Kuhusu Maambukizi ya Virusi Vya Corona:
Kumekuwepo na mkanganyiko wa taarifa juu ya chanzo, maambukizi na kinga dhidi ya virusi vya Corona. Mtandaoni na kwenye vyombo vya habari taarifa za ukweli zikiwa zimechanganyana na kiasi cha uongo.
Kiukweli hamna mtu anayepaswa hasa kulalamikiwa kutokana na ukweli kuwa maambukizi ya Virusi vya Corona bado ni jambo geni.
Basi kwa leo, kutokana na utafiti mdogo wa ufuatiliaji niliofanya, nitajaribu kurekebisha baadhi ya taarifa zisizo sahihi zinazosambaza kuhusu maambukizi ya virusi vya Corona.
Je ni ukweli ugonjwa wa Virusi vya Corona hauwezi kumdhuru mtu mweusi?
Ukweli ni kuwa mtu mweusi hana kinga mwili dhidi ya virusi vya Corona. Anaweza pata maambukizi kama mtu yeyote mwingine yeyote. Hili linadhihirika kwa watu weusi maarufu kadhaa ambao wamepimwa na kukutwa na virusi vya Corona, kama Callum Hudsoi-Odoi mchezaji wa Chelsea, Omar Colley kutoka timu ya Sampdoria, bila kusahau wachezaji kikapu Christian Wood na Donovan Mitchell kutoka marekani, nikichukua baadhi tu.
Lakini hapa wengine husema hata kama tukipata maambukizi, mtu mweusi hawezi onyesha dalili na kuweza dhurika na ugonjwa huo wa Corona. Ukweli ni kuwa kama mtu anaweza kuambukizwa na virusi hivi, basi hatari ya kuweza kuonyesha dalili na kuweza kudhurika na ugonjwa huu ipo.
Je ni kweli ugonywa wa Corona unaambukizwa kwa njia ya Hewa?
Ukweli ni kwamba ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona hausambazwi kwa njia ya hewa. Ugonjwa huu sio Airborne. Ugonjwa huu huambukizwa kwa njia yam atone tone yanayotakana na mtu mgonjwa kupiga chafya kama uko umbali wa karibu na mgonjwa, kushika kamasi au kugusana mikono na mgonjwa ambaye ambaye ametoka kuambukiza mikono yake. Unaposalimia nae kwa mikono na kisha kugusa pua ama mdomo wako, virusi hivyo ndipo huingia kwa mfumo wa hewa na kuleta maambukizi kwa mwili.
Je ni kweli ugonjwa wa Corona ni wa kuwatengenezwa maabara na umeambukizwa kwa kupandikizwa nchini China?
Hapana, huu nao siyo ukweli. Asili ya ugonjwa huu ni kiumbe popo. Virusi hivi si vipya na havijatengenezwa maabara, mbali viliambukizwa kutoka kwa popo kwenda mnyama wa kati na kisha kumfikia binadamu kupitia mkutano na mnyama huyo. Hamna ushahidi unaomuhusisha Marekani wala nchi yeyote ingine ile, katika namna ugonjwa huu umetokea na kusambaa.
Je ni kweli virusi vya Corona ni virusi vipya?
Hapana, huu nao si ukweli, Virusi vya Corona ikiwemo COVID19 ni aina flani za virusi vilivyo katika kundi moja la familia za virusi vinavyoitwa Corona.
Kwa hivi karibuni, aina flani ya virusi vya Corona vimeshawahi kusababisha mlipuko wa magonjwa ya mafua ya ndege unaofanana kwa kiasi na ugonjwa huu wa sasa, ulisababisha SARS mwaka 2003, na MERS mwaka 2012.
Ugonywa huu una Tiba
Ukweli ni kuwa hadi sasa ugonjwa huu hauna tiba, matibabu huzingatia dalili zinavyokuwa na watabibu hutoa huduma stahiki kulingana na hali inavyokuwa.
Juhudi zinafanyika kutafuta chanjo na tiba stahiki, lakini mpaka sasa hili ni jambo la kusubiri.
Afrika haiwezi kupata mlipuko mkubwa wa ugonjwa kama ilivyotokea ulaya
Kutoka na utofauti wa hali ya hewa kati ya ulaya nan chi za Afrika kuna watu wana Imani kuwa, Virusi vya corona haviwezi kushamiri na kusababisha mlipuko mkubwa wa maambukizi kama ilivyokuwa kwa wenzetu wan chi za ulaya.
Ukweli unabaki kuwa, jambo hili halina ushahidi wowote wa kiutafiti, na ukizingatia miundombinu yetu ya kiafya, kinga ni bora kuliko tiba. Ni kheri kujidhatiti katika kujikinga, na kuepusha kupata maambukizi kuliko kujifariji na Imani hii.
Virusi vya Corona haviwezi kuzuilika nchi za Afrika hata kama tukichukua hatua
Hili nalo si kweli, pamoja na mapungufu yetu ya miundombinu yetu ya afya, kila mtu akijidhatiti na kuwa makini, tuna uwezo wa kulikwepa na kujiepusha na janga hili.
Kama ambavyo nchi kadhaa za afrika zimegundua maambukizi na kuanza kuweka mipango ya kukabiliana na gonjwa hili, nchi zingine hazina budi kujifunza kutoka kwa wenzetu.
Haya ni mambo machache niliyosikia kuhusu maambukizi ya Virusi vya corona ambayo sikuona yakiwa yamekaa sawa. Nimeyajibu na kuyatolea ufafanuzi kwa kadri ya uelewa wangu. Je wewe ni mambo gani mengine umeyasikia kuhusu virusi vya Corona ambayo unahisi hayako sahihi?
Music used is from YouTube Audio Library. All images used are for educational purpose only.
#Homa #Corona #Afrika
Ещё видео!