#HabarizaUN #UmojawaMataifa #Kiswahili #UNNewsKiswahili
Kampeni ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu iliyoanza tarehe 25 mwezi huu huko Kivu Kaskazini nchini jamhuri ya Kidemokraia ya Congo, DRC imemalizika jana Jumatatu ya tarehe 30.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO lilizindua kampeni hiyo ya chanjo kwa wakimbizi wa ndani katika kambi ya wakimbizi hao ya Kanyaruchinya wilayani nyiragongo katika mji wa Goma jimboni Kivu Kaskazini ambapo walengwa wameshukuru WHO kutokana kwamba ungonjwa wa kipindupindu ni moja ya shida zinazowakabili. Mwandishi wetu wa DRC Byobe Malenga ambaye ameshuhudia harakati za utoaji chanjo alifika eneo na kuandaa mada hii ifuatayo
Ещё видео!