Dk Tulia Ackson ametangazwa rasmi leo Jumanne Februari Mosi kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kushunda kwa kupata kura zote 376 zilizopigwa.
Akisoma matokeo hayo, aliyekuwa Waziri wa Ardhi, William Lukuvi amesema kuwa wagombea wengine wanane hawakupata kura hata moja na kwamba hakuna kura iliyoharibika.
Mwenyekiti wa uchaguzi William Lukuvi amemtangaza mgombea huyo wa CCM muda mchache baada ya kura kuhesabiwa
![](https://s2.save4k.ru/pic/om50UZcGb7c/maxresdefault.jpg)