DUMISHENI UTAMADUNI WA KUAGANA - Dkt. STERGOMENA
Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb), amewataka Maafisa na Askari kuendelea kudumisha utamaduni waliojiwekea wa kuagana kwa lengo la kutambua mchango wao kwa Jeshi na Taifa kwa ujumla. Utaratibu huu unasaidia kuleta mshikamano na kuendeleza umoja. Wito huo umetolewa na wakati wa hafla fupi ya kuwaaga Majenerali wastaafu hafla iliyofanyika Ukumbi wa Makuti Msasani Beach.
“Mambo ya kujivunia katika Jeshi letu la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Ni kujaliwa kuwa na Maafisa na Askari waliojaa uzalendo na utii wa hali ya juu. Uzalendo wao na kujituma kwao kumewezesha Taifa letu kuendelea kuwa na amani na utulivu, Ni dhahiri kuwa Majenerali hawa tunaowaaga hivi leo wametoa mchango mkubwa katika kuliheshimishaTaifa letu. Mchango walioutoa hauna budi kuendelea kuenziwa”, alisema.
Kwa upande wake, Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Salvatory Venance Mabeyo amesema “Majenerali hawa wamestaafu baada ya kutimiza umri wa lazima kwa Mujibu wa Sheria. Mchango wa Majenerali hawa wanane tunaowaaga leo wameutoa katika kufanikisha utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Jeshi letu na maendeleo tuliyoyapata.”
Katika kipindi cha utumishi wao wamelitumikia Jeshi letu na Taifa kwa uzalendo wa hali ya juu ndani na nje ya nchi. Wamenesha uzalendo, uadilifu na weledi na nidhamu katika vyeo na nyadhifa mbalimbali.
#wizarayaulinzi #jwtz #jkt
Ещё видео!