Mtoto Leonard Morisha mwenye umri wa miaka 11 hivi sasa ,aliyefariki dunia juni 27 mwaka 2017 katika hospitali ya Wilaya ya Geita alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa ugonjwa wa kuishiwa damu na kuzikwa nyumbani kwao kijiji cha Ngema Wilayani Mbogwe mkoani Geita ,amepatikana akiwa hai.
Mtoto Leonard Morisha alionekana kwa mara ya kwanza octoba mwaka huu majira ya usiku katika kijiji cha Segese ,Msalala Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga akiwa mzima,akirandaranda kwenye maduka,ndipo mlinzi aitwae Emmanuel Busiga alimchukua na kumpeleka nyumbani kwake.
Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la polisi mkoani Geita KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI HENRY MWAIBAMBE .amesema juhudi za kumtangaza mtoto huyo zilizaa matunda baada ya kufanikiwa kuwapata wazazi wa mtoto huyo.
Ещё видео!