Leo March 14, 2018 Mwanajeshi MT 109795 Private Ramadhan Mlaku mwenye umri wa miaka 28 amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la mauaji ya askari mwenzie, MT 79512 SGT Saimon Munyama.
Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakama hapo akiwa kwenye gari la Jeshi la kubebea wagonjwa huku akiwa na majeraha miguuni.
Akisomewa shtaka lake na Wakili wa Serikali, Mosie Kaima mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba amedai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kosa moja la mauaji.
Inadaiwa mshtakiwa huyo ambaye ni Mwanajeshi wa Kambi ya Jeshi Makongo ametenda kosa hilo October,30, 2017 akiwa Makao Mkuu ya JWTZ Upanga Ilala Dar es Salaam ambapo alimuua askari mwenzie MT 79512 SGT Munyama.
Ещё видео!