Muungano wa Vyama vya Siasa vya Upinzani (14),nchini umejitenga na msimamo ulitolewa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wanaodai hakukuwa na umuhimu wa kuundwa kwa kikosi Kazi Kilichokuwa kinakusanya maoni kutafuta muafaka wa kitaifa ulitokana na mkwamo wa kisiasa.
Jana,Oktoba,22,2022 Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika aliitaka Serikali kuweka wazi gharama ambazo kikosi hicho kimetumia huku akisema hakukuwa na haja ya kutafuta maoni ya wananchi kwani kazi iliishafanywa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.
Mgawanyiko huo wa kimtazamo kwa Vyama hivyo vinavyotegemea kuja na sera mbadala dhidi ya Chama tawala, unatokea ikiwa ni siku mbili baada ya kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wananchi kuhusu demokrasia ya vyama vingi, kukabidhi ripoti yake kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
Wakizungumza leo,Oktoba23,2022,Kwa niaba ya Muungano huo,Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo amesema hawaungi mkono hoja zilizotolewa na Chadema na kwamba wamekurupuka kujenga hoja bila kufanya utafiti.
![](https://i.ytimg.com/vi/rvtHEzvE_2o/maxresdefault.jpg)