268 #Nyimbozawokovu
268
1. E’ Yesu, ingia rohoni kabisa,
uniweke huru nakunitakasa,
nipate kushirikiana na wewe
katika mateso na raha daima!
Pambio:
:/: E’ Bwana, nijaze
upendo wa mbingu
nao uthabiti,
niwe mshindaji! :/:
2. Siombi ufalme, siombi heshima,
naomba kupewa neema daima,
nijue ukweli wa neno la Mungu:
Mtoe miili na iwe dhabihu!
3. Ingia rohoni, unichungulie,
na katika yote unisaidie,
nipate kabisa kusudi na nia
kujitoa kwako, kukutumikia!
4. Hakuna la huku litanizuia
nisifananishwe na Yesu Masiya.
Nitumainije kufika mbinguni
nisiposhiriki Mwokozi mpendwa!
![](https://i.ytimg.com/vi/s4zQijyKMUo/mqdefault.jpg)