Maofisa wa Polisi ambao wanatuhumiwa kwa mauaji ya Mfanyabiashara wa madini Mkoani Mtwara, Musa Hamis wamepandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mtwara huku ulinzi wa Polisi ukiwa umeimarishwa ndani na nje ya Mahakama.
Waliofikishsa Mahakamani ni Mrakibu wa Polisi Gilbert Kalanje (Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Mtwara), Mrakibu Msaidizi wa Polisi Charles Onyango (Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara), Mrakibu wa Polisi Msaidizi Nicholaus Kisinza (Mkuu wa Kikosi cha Intelejensia ya Jinai Mkoa wa Mtwara), Mkaguzi wa Polisi John Msuya Mganga (Mkuu wa Zahanati ya Polisi Mtwara), Mkaguzi wa Polisi Msaidizi Marco Mbuta, Mkaguzi wa Polisi Shirazi Mkupa na Koplo Salimu Juma Mbalu.
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Lugano Kasebele ameahirisha kesi hadi Februari 22,2022 itakaposikilizwa tena.
![](https://i.ytimg.com/vi/sAoE03xs4NI/mqdefault.jpg)