#HabarizaUN #UmojawaMataifa #Kiswahili #UNNewsKiswahili
Ikiwa leo hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa Jukwaa la kisiasa la ngazi ya juu la Umoja wa Mataifa HLPF kuhusu malengo ya maendeleo endelevu SDGs limeingia siku yake ya nne na linategemewa kuendelea hadi tarehe 17 ya mwezi huu wa Julai, nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wametuma wawakilishi kutoka katika serikali zao ili kushiriki mkutano huu muhimu. Je, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Tanzania imewasilisha nini kwenye jukwaa hili? Katika mahojiano na Anold Kayanda wa Idhaa hii, Katibu Mkuu Mhandisi Cyprian John Luhemeja anaeleza.
Ещё видео!