FAIDA 5 ZA KUCHUMA JUANI KATIKA KUSOMA VITABU NI UFAHAMU WA MENGI KAMA MJUSI ANAVYOJUA JOTO LA JIWE Ni video makini sana katika kukuelimisha faida za kuchuma JUANI KATIKA KUSOMA VITABU.
Zifuatazo ni faida 5 za kuchuma JUANI KATIKA KUSOMA VITABU.
1.Ndiyo HAZINA isiyokauka.
Walt Disney alisema "There is more treasure in books than in all the pirate's loot on treasure Island".
Kama unataka kuiba na usikamatwe,kama unataka kuiba na unachoiba kidumu na wewe milele,basi soma vitabu.
Kwa nini? Kwa sababu unaposoma, unapata kwa urahisi kile ambacho kimemchukua MTU mwingine miaka mingi kukipata.
Mfano MTU amejaribu biashara 10 zikashindwa,ila ya 11 ndiyo ikafanikiwa.
Akaandika kitabu kinachoeleza makosa aliyofanya kwenye biashara 10 zilizoshindwa na wewe ukakisoma,Unakuwa umeiba,Unakuwa umeepuka kurudia makosa yake na hivyo utapiga hatua kubwa.
VITABU ndiyo HAZINA pekee isiyokauka,hazina ambayo ukiweza kuiiba hakuna atakayekukamata na hakuna anayeweza kukuibia na ni HAZINA ambayo inapatikana kwa urahisi popote pale ulipo.
2.Unawajua marafiki wa kweli.
Abraham Lincoln alisema " My best friend is a person who will give me a book I have not read ".
Watu huwa wanalalamika kwamba hakuna marafiki wa kweli au ni vigumu kuwajua marafiki wa kweli.
Hii ni kwa sababu mtu anapokuwa na mafanikio anazungukwa na watu wengi, Lakini akishindwa hawaoni tena wale marafiki aliokuwa nao.
Unapokuwa msomaji ni rahisi sana kuwajua na kuwapata marafiki wa kweli, kwa sababu wanakuwa ni wale ambao wanakupa VITABU ambavyo hujasoma.
MA una marafiki ambao ukiwaambia unasoma VITABU wanakushangaa na kukuambia unapoteza muda,jua hao siyo marafiki wa kweli, wako na wewe kwa sababu kuna kitu wanapata.siku watakosa kitu hicho,hutawaona tena.
Kuwa msomaji na wafanye watu wajue wewe ni msomaji na hapo utaweza kuwajua marafiki wako wa kweli kwa VITABU watakavyokuwa wanakupa au wanakuambia usome.
3.Unasafiri bila kutoka hapo ulipo.
Mason Cooley alisema " Reading gives us some place to go when we have to stay where we are ".
Moja ya njia za kuijua vizuri dunia ni kusafiri sehemu mbalimbali duniani.Lakini siyo wote kwenye uwezo au wanaopenda kusafiri.
Kusoma ni njia rahisi ya wewe kusafiri bila kuondoka hapo ulipo sasa.
Unaposoma VITABU unajenga taswira mbalimbali, kama ni riwaya unatengeneza picha ya matukio kwenye akili yako.
Kama ni historia ya MTU unapata picha ya maisha ambayo MTU huyo aliishi,ni kama Unakuwa umeishi maisha hayo pamoja na yeye.
Unaposoma kitu chochote, akili yako haitabaki kama ilivyokuwa mwanzo,ambapo ni sawa na unaposafiri kwenda sehemu yoyote.
Hivyo kuwa msomaji, utafika maeneo mengi bila hata ya kusafiri.
4.Ni zoezi kwa akili yako.
Richard Steele alisema " Reading is to the mind what exercise is to the body".
Moja Kati ya sheria za mageuzi inasema kwamba kitu kinapotumiwa kinakuwa imara na kisipotumiwa kinakuwa dhaifu.
Mfano mzuri ni mikono yako,kama huwa unatumia zaidi mkono wa kulia kufanya vitu, Unakuwa na nguvu kuliko mkono wa kushoto.
Kadhalika Kama unatumia zaidi mkono wa kushoto.
Hivyo pia ndivyo ilivyo kwa akili yako, kama unaitumia inakuwa imara,kama huitumii inakuwa dhaifu.
Njia pekee ya kuitumia akili ni kuipa zoezi LA KUSOMA VITABU.
Unaposoma VITABU unaipa akili yako kazi ya kufikiria na kutengeneza taswira mbalimbali na hilo linaifanya akili yako kuwa bora zaidi.
Unapokuwa msomaji akili yako inakuwa imara na yenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa urahisi kwa sababu imeshazoea kufikiri vitu vigumu na vikubwa.
Usikubali akili yako iwe dhaifu, ifanye kuwa imara kwa kuwa msomaji.
5.Unajitofautisha na wasiojua kusoma.
Kuna msemo unaosema "The man who doesn't read has no advantage over the man who can't read".
Kama unajua kusoma Lakini husomi VITABU, huna tofauti na MTU asiyejua kusoma.
Wote mtasumbuka kwa jambo linalofanana wakati majibu ya jambo hilo yapo kwenye VITABU.
Kuwa msomaji na utaweza kujitofautisha sana na wengine ambao hawajui kusoma au hawataki kusoma.
FAIDA 5 ZA KUCHUMA JUANI KATIKA KUSOMA VITABU NI UFAHAMU WA MENGI KAMA MJUSI ANAVYOJUA JOTO LA JIWE Ni video ambayo itakupa matokeo makubwa katika kujenga tabia ya kusoma VITABU.
Zifuatazo ni link za kusoma VITABU.
1.SOMA VITABU TANZANIA.
w.w.w.t.me/somavitabutanzania.
2.Kupata VITABU vizuri vya kusoma tembelea.
w.w.w.amkamtanzania.com/vitabu.
Kwa mawasiliano.
Simu:0758602036.
Instagram @Hosea Simwogope.
Facebook @Hosea Simwogope.
Twitter @Hosea.
Email:hoseasimwogope@gmail.com.
Ещё видео!