#MsasaUpdates KATI YA 17 WALIOFARIKI AJALI YA TANGA 14 NI WA FAMILIA MOJA...
Kati ya Watu 17 waliofariki ajali ya Tanga 14 ni wa familia moja ambapo kwenye ajali hiyo wengine 12 wamejeruhiwa.
Ajali hiyo imetokea eneo la Magira Gereza, Tarafa ya Mombo wilaya ya Korogwe mkoani Tanga.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amesema Ajali hiyo imehusisha gari aina ya Mitsubishi Fuso iliyoligonga gari aina ya Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 ikitokea jijini Dar es Salaam kwenda Moshi kwa ajili ya mazishi.
Waliofariki kwenye ajali hiyo ni wanaume tisa, wanawake sita, watoto wawili mmoja wa kike na mmoja wa kiume.
Majeruhi 10 wamehamishiwa Hospitali ya
Rufaa ya Mkoa wa Tanga, Bombo kuendelea na
matibabu na wawili wamebaki Hospitali ya Wilaya
Magunga huku hali zao zikiendelea vizuri. Mgumba amesema miili ya marehemu ipo katika Hospitali ya Wilaya Magunga, Korogwe.
Chanzo cha ajali ni kimeripotiwa kuwa ni uzembe wa dereva wa gari aina ya fuso kutaka kulipita gari lililokuwa mbele yake na ndipo lilipogongana uso kwa uso na Coaster hiyo.
Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi.
Ahsante kwa kuwa mwana familia, kwa habari murua utazipata hapa, Ungana nasi kwa kila update zitakazo jitokeza.. Subscribe Channel yetu ili usipitwe na habari zetu.
#tanzania #ajali #ajaliyatangaleo
Ещё видео!