Kama wewe kweli, adui yako ni umasikini, Mara baada ya kupata ujuzi na kuwa na uhakika wa kupata kipato chako cha kuendesha maisha. Kama ukiwa na maarifa ya fedha, na ukajifunza kuwa na jicho la kuona fursa.
Kuna vingi vya kufanya kupitia kipato chako, kuna vingi vya kufanya kupitia faida zako ili uweze kusonga mbele zaidi kwenye maisha, na kuukimbia umasikini.
Sasa basi, leo katika video hii. Ntajaribu kukupatia maarifa fulani machache ambayo ni ya kawaida, lakini kama utayazingatia, yanaweza kukubadilishia maisha yako, kupitia kipato hicho hicho kidogo unachokipata, na kukutoa kwenye hatua moja na kukupeleka hatua nyingine.
Ili baada ya miaka mingi, kwa juhudi, nidhamu na jasho lako, uwe mmoja ya watu walioupinga umasikini kwenye maisha yao.
Somo la kwanza ambalo kwangu naliona ni la muhimu kupita yote, linapokuja swala la maarifa mazuri ya fedha, ni ujuaji wa kuweka Akiba na ujuaji wa kuikuza Akiba. Labda kwa kuanza, ngoja nijaribu kuielezea akiba ni nini?
Akiba ni kiwango kidogo cha fedha unachohifadhi kila mwezi au baada ya muda fulani, kutoka kwenye kipato au mapato yako, kwa malengo ya, aidha kuitumia Akiba huyo, utakapopata dharula au kama mbinu ya kujenga na kukuza mtaji.
Ili baadae, utakapoona kiasi kinatosha. Sasa uanze kujaribu aidha wazo la biashara au uwezekaji ambao ulikuwa unatamani kuufanya kwa muda mrefu, kama mbinu ya kutengeneza kipato cha pili, pembeni ya shughuli yako mama.
Sasa unaweza kuuliza. Je ntawezaje kuweka Akiba? Je kuweka Akiba, ni kitu nachoweza kujifunza? Kumbuka mfano wa muuza mikanda. Kama ambavyo tulizungumzia umuhimu wa kudhibiti gharama za uendeshaji wa biashara ya ili muuza mikanda aweze kuona faida na pia asile mtaji.
Vivyo hivyo hichi kitu hichi, kinapaswa kufatwa hivyo hivyo na mfanyakazi. Mfanyakazi, naye kama mfanyabiashara , ili apige hatua, lazima gharama zake za maisha ziwe chini ya kipato anachoingiza kwa mwezi.
Na ndo mana, mfanyakazi huwa anaambiwa Aishi maisha kulingana na uhalisia wa kipato chake. Kama mshahara wako ni laki tatu, ili uweze kuona hela ya kuweka Akiba, ishi maisha ya laki tatu na siyo ya laki sita.
Kuishi chini ya kipato unachoingiza ndo Siri pekee ya kuweza kuweka Akiba. Ndi kanuni mama ya kujikwamua na umasikini mara unapokuwa na uhakika wa kipato.
Lakini unaweza kulalamika kuwa, hauwezi weka Akiba kwa sababu mashahara wako ni mdogo. Ingawa hili Lina ukweli, na mishahara yetu ni midogo, bado hatuna budi ya kujua namna ya kuweza kulizingatia hili, hasa kipindi unapoona kuwa hili haliwezekani.
Unachotakiwa kufahamu ni kuwa, kuna watu wana kipato chini zaidi yako lakini Bado wanaishi, na bado kwenye hicho hicho kidogo, wanaweka na Akiba. Penye nia pana njia.
Lakini jambo la pili, kuweka Akiba, Siri yake siyo lazima, uanze kwa kuweke hela kubwa sana kila mwezi. La hasha! Siri ya kujifunza kuweka Akiba, ni kuanza kuweka kile kiasi ambacho una uwezo nacho kulingana na malipo yako.
Kama mshahara wako ni laki mbili. Weka hata Akiba ya elfu Tano kwa mwezi, kwa kuanzia. Lengo la mwanzoni unapoanza kuweka Akiba. Fokasi siyo kiasi unachoweka, fokasi inapaswa kuwa kwenye kujenga tabia ya wewe kuweza kuweka akiba.
Ukiweza weka Akiba kiasi kidogo, kadri miezi inavyokwenda, utazoea na kujenga tabia mpya. Na unapokuwa ushajenga tabia mpya ya kuweka Akiba, unaweza sasa, ongeza kiwango cha hela unachoweka Akiba kidogo kidogo, kadri unavyohimili. Na muda si muda utajikuta umeweka kiasi cha kikubwa bila kuamini kama ingewezekana.
Ingawa wazo hili ni jepesi kwa nilivyolielezea hapa, lakini utekelezaji wake huwa ni mgumu sana, na watu wengi hiki kitu huwashinda. Lakini kama unataka kujikwamua na umasikini na umefikia hatua ya kujiingizia kipato, kuweza kuweka Akiba ni Siri mojawapo ya kuweza kujikwamua na umasikini
#umasikini #ujuzi #fedha
Ещё видео!